Psalms 130:4-8

4 aLakini kwako kuna msamaha,
kwa hiyo wewe unaogopwa.

5 bNamngojea Bwana, nafsi yangu inangojea,
katika neno lake naweka tumaini langu.
6 cNafsi yangu inamngojea Bwana
kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi,
naam, kuliko walinzi
waingojeavyo asubuhi.

7 dEe Israeli, mtumaini Bwana,
maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma,
na kwake kuna ukombozi kamili.
8 eYeye mwenyewe ataikomboa Israeli
kutoka dhambi zao zote.
Copyright information for SwhNEN